Nionapo amani kama shwari,
Ama nionapo shida;
Kwa mambo yote umenijulisha,
Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

Ingawa Shetani atanitesa,
Nitajipa moyo kwani;
Kristo ameona unyonge wangu,
Amekufa kwa roho yangu.

Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

Dhambi zangu zote, wala si nusu,
Zimewekwa Msalabani;
Wala sichukui laana yake,
Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

Ee Bwana himiza siku ya kuja,
Panda itakapolia;
Utakaposhuka sitaogopa,
Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.