Cha kutumaini sina,
Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha,
Dhambi zangu kuziosha.


Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama.


Njia yangu iwe ndefu,
Yeye hunipa wokovu,
Mawimbi yakinipiga,
Nguvu ndizo nanga.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama.

Damu yake na sadaka,
Nategemea daima,
Yote chini yakiisha,
Mwokozi atanitosha.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama.

Nikiitwa hukumuni,
Rohoni nina amani,
Nikivikwa haki yake,
Sina hofu mbele zake.

Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama,
Ndiye mwamba ni salama.