Nitamshukuru Mungu,
Kwa upendo wake mkuu,
Alimtuma Mwanawe,
Kunifilia mimi.

Kweli nitaimba nyimbo,
Za upendo wake mkuu,
Pamoja na malaika,
Walioko mbinguni

Nalifanya dhambi nyingi,
Nilikaa maovuni,
Bali nimeokolewa,
Yesu hunisafisha.

Kweli nitaimba nyimbo,
Za upendo wake mkuu,
Pamoja na malaika,
Walioko mbinguni

Amenipa Roho yake,
Anijaze daima,
Nimekuwa mwana wake,
Hunipenda kabisa.

Kweli nitaimba nyimbo,
Za upendo wake mkuu,
Pamoja na malaika,
Walioko mbinguni

Mungu wangu, nashukuru
Husujudu daima,
Neno lako nitangaze,
Kwa upendo popote.

Kweli nitaimba nyimbo,
Za upendo wake mkuu,
Pamoja na malaika,
Walioko mbinguni