Njoni na furaha, Enyi wa Imani,
Njoni Bethlehemu upesi!
Amezaliwa mjumbe wa Mbinguni
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.

Mungu wa waungu, Mwanga wa mianga,
Amekuwa radhi kuzaliwa;
Mungu wa kweli, wala si kiumbe
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.

Jeshi la mbinguni, Imbeni kwa nguvu!
Mbingu zote na zijae sifa!
Sifuni Mungu aliye mbinguni;
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.

Ewe Bwana Mwema, Twakubarikia,
Yesu, utukufu uwe wako;
Neno la Baba limekuwa mwili;
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.